Akizungumza mwishoni mwa mkutano
wa viongozi wa Umoja wa Afrika, Kamishna wa Amani na Usalama wa Umoja huo,SMAIL
CHERGUI aliwaambia waandishi wa habari kwamba kazi ya ujumbe wa wataalamu hao
50 wa kijeshi itakuwa kuangalia nini kinachotokea na kama itahitaji kutoa
ushauri nasaha kwa polisi.
Hivi sasa Bwana NKURUNZIZA
anakabiliwa na shinikizo la kimataifa kufikiria upya uamuzi wake ambao
wanadiplomasia wanahofu unaweza kuitumbukiza nchi hiyo kwenye vita vya wenyewe
kwa wenyewe ambapo hadi sasa machafuko ya Burundi yamesababisha vifo vya watu
40 na wengine 100,000 kukimbilia nchi jirani.
Uchaguzi wa Bunge umepangwa
kufanyika tarehe 29 mwezi huu kabla ya uchaguzi wa rais mwezi ujao na tume ya
uchaguzi imeidhinisha wagombea wote wanane waliojitokeza kugombea uchaguzi wa
rais akiwemo Bwana NKURUNZIZA na mpinzani wake mkubwa Bwana AGATHON RWASA.
0 comments:
Post a Comment