Rais KIKWETE ameyasema hayo
wakati wa usinduzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuulia viluwiluwi vya
mbu wanaoeneza malaria kilichoko katika eneo la viwanda la TAMCO wilayani
Kibaha.
Amevitaja vipaumbele hivyo kuwa
ni kutumia dawa mseto kutibu wagonjwa wa malaria. kuhamasisha matumizi ya
vyandarua vilivyopuliziwa dawa na kupulizia dawa inayoua mbu ndani ya nyumba.
Amesema kwa kufanya hivyo kiwango
cha maambukizi nacho kimepungua kutoka asilimia 18 mwaka 2007 hadi asilimia 10
mwaka 2012. Aidha, vifo vitokanavyo na malaria kwa wazazi vimepungua kutoka 41
kwa vizazi hai laki moja mwaka 2004 hadi 12 kwa vizazi hai laki moja mwaka 2014.
Rais KIKWETE amesema idadi ya
wagonjwa wenye umri wa chini ya miaka mitano imepungua kutoka zaidi ya wagonjwa
milioni tano mwaka 2004 hadi zaidi ya
wagonjwa milioni tatu mwaka 2014 na vifo vya watoto wa miaka mitano kwenda
chini vimepungua kutoka zaidi ya laki saba mwaka 2004 hadi zaidi ya laki nne
waka 2014.
Amesema kwa ujumla idadi ya
wagonjwa wote imepungua kwa asilimia 51 na vifo kwa asilimia 71 kati ya 2004 na
2014.

0 comments:
Post a Comment