Mkurugenzi Mpya wa kampuni ya The Guardian Richard Mgambwa akionekana hapo baada ya kukabithiwa ofisi hivi leo.
Kampuni ya The Guardia LTD hii leo
imeweza kupata mkurugenzi Mtendaji mpya Bwana Richard Mgamba hatua ambayo
imepokelewa vyema na wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Mapema leo Shughuli hiyo ya kumpata
Mkurugenzi huyo mpya Bwana Mgamba baada
ya kiti hicho kuwa wazi kwa muda baada ya Aliyekuwa Mkurugenzi wa Kampuni Hiyo
Kustaafu Bwana Kiondo Mshana mwishoni mwa
mwaka jana 2014 imefanywa na mwenyekiti wa makampuni ya IPP Dakta.Reginard
Mengi katika ofisi hizo za the Guardiani mikocheni jijini Dar es Salaam.
Shughuli ya kukabidhi ofisi hiyo
imefanywa na Mkurugenzi mtendaji wa ITV na Radio One Joyce Mhavile ambaye ndiye
aliyekuwa ameshika nafasi hiyo kwa kipindi cha miezi sita yaani kuanzia mwezi
january hadi june 2015 kabla ya kuteuliwa kwa mkurugenzi mpya huyu Bwana
Richard Mgamba anayeanza kazi rasmi hivi leo.
Mkurugenzi mtendaji wa ITV na Radio One Joyce Mhavileakiwa katika ofisi za Guardian Baada ya Kumkabidi Bwana.Richard Mgamba ofisi ilikuendelea na majukumu.
Wakizungumza mara baada ya
mkurugenzi mpya kukabidhiwa ofisi na kuanza kazi mara moja, baadhi ya viongozi
wa kampuni ya The Guardian LTD wamesema kuteuliwa kwa Bwana.Mgamba kuwa
Mkurugenzi mtendaji wa The Guardian itasababisha kampuni hiyo kuendelea kufanya
vizuri zaidi kutokana na uwezo mkubwa wa mkurugenzi huyo na hivyo imani
waliyokuwa nayo ni kubwa.
Kwa upande wa wafanyakazi wa
kampuni ya The Guardian LTD Wameieleza Tambarare
Halisi kuwa wamepokea kwa mikono miwili uteuzi wa mkurugenzi huyo
Bwana.Richard Mgamba kutokana na ukweli kwamba ni mwenye uwezo wa kung”amua
mambo haswa kwa ustadi mkubwa na ikiwa kavitumikia vyombo hivi vya habari kwa
muda mwingi hivyo analojicho la kipekee la kuhakiki kuwa kampuni hiyo inapaa
zaidi na zaidi na inaendelea kuwa na heshima hivyo ushirikiano watamuonyesha
kwa kiwango kikubwa katika utendaji kazi wake.
Wafanyakazi wa The Guardian wakibadilishana mawazo na Mwenyekiti Mtendaji Mpya Bwana Richard Mgamba ofisini hapo baada ya kukabithiwa ofisi Rasmi ili aanze kazi.
Katika hatua nyingine Mkurugenzi
huyo mpya wa The Guardian Bwanana Mgamba ambaye Tambarare Halisi ilitaka kufahamu mapokeo ya ukurugenzi huo nay eye
namna alibvyo jipanga lipoje?.
Bila hata kumumunya maneno amesema
kuwa”Nitafanya kazi kwa ustadi wa hali ya juu kwa nafasi hii niliyo aminiwa na
kupewa hivi leo na naanza kazi rasmi hivyo imani yangu ni kuhakikisha Kampuni
hii inasonga mbele zaidi na vuilevile kuhakikisha kazi inafanyika kwa
ushirikiano uliyo thabiti kwani wafanyakazi na viongozi wameonyesha imani
kwangu”Alisema Mgamba.
Bwana Mgamba
kabla ya kujiunga na Guardian Amekuwa Mhariri Mtendaji katika gazeti la Citizen
linalotolewa na Mwananchi Communications.
Baada ya Hafla hiyo fupi ya kupewa
na kukabidhiwa kiti alichokuwa awali anacho Bwana Kiondo Mshana kabla ya kustaafu
na kupewa Mkurungenzi Mtendaji ITV/Radio one Joyce Mhavile ambaye alikuwa
kashika ofisi hiyo kwa muda Tambarare Halisi imeshuhudia Nyuso za
Furaha kwa wafanyakazi waliokuwapo eneo hilo huku kwa nyakati tofauti kila
mmoja akimzungumzia Bwana Mgamba kwamba sasa wamepata chaguo zuri na ambalo
kila mmoja ameliafiki bila kung”ata maneno hivyo safari itakuwa njema kwao na
itakayo fanya kazi iende sawa bini sawia, kwakuwa ni mtu ambaye ataleta mabadiliko
makubwa katika ya kampuni na tasnia ya habari hapa nchini kiujumla bila ya
kupepesa macho.
#Hii ni sehemu ya #viongozi na wafanyakazi wakieleza walivyo mpokea #Tizama.
#Hii ni sehemu ya #viongozi na wafanyakazi wakieleza walivyo mpokea #Tizama.




0 comments:
Post a Comment