Image
Image

News Alert:Wagombea wapinga uchaguzi.


Sakata la baadhi ya wagombea ubunge katika maeneo mbalimbali hapa nchini kulalamikia mchakato wa kura za maoni kwa madai ya kutotendewa haki na kukiuka kanuni za uchaguzi limeendelea kutikisa.

Wagombea tisa kati 12 wa Jimbo la Namtumbo wamejitokeza kupinga kurudiwa kwa upigaji wa kura za maoni upya katika jimbo hilo huku wakimuunga mkono mgombea aliyeshinda,Bwana VITA KAWAWA.

Wagombea ubunge hao wakiwakilisha wenzao wengine watano, wameibukia katika Ofisi za Chama cha Waandishi wa Habari Mjini Songea Mkoa wa Ruvuma, wakiwa na barua mbalimbali za malalamiko wakiupinga uongozi wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Namtumbo kurudia tena zoezi la upigaji kura za maoni wakidai kura hizo zinalenga kumbemba mgombea mmoja wapo aliyeshindwa katika mchakato huo.

Wanasema hawakubaliani na viongozi hao wa CCM Namtumbo kulazimisha kurudia zoezi hilo ili kumpitisha mgombea wao wanayemtaja kwa jina la EDWIN NGONYANI na kwamba wapo tayari matokeo ya mwanzo yaendelee,  ambayo yalimpa ushindi mbunge aliyekuwa akitetea nafasi yake, VITA KAWAWA.

Katibu wa CCM Wilaya ya Namtumbo ambaye pia ni Mkurugenzi wa uchaguzi wa wilaya hiyo, Bwana ABDULAZIZ MOHAMED anasema hizo ni propaganda za wagombea na kwamba marudio ya uchaguzi yapo pale pale.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment