Image
Image

JPM arejesha sura 13, atema 13 wa Kikwete.

RAIS John Magufuli amerejesha sura 13 zilizokuwemo kwenye Serikali ya Awamu ya Nne, ambao sasa wanaunda Baraza lake la Mawaziri la watu 34 na kuwatupa mawaziri wengine 13 walioshinda ubunge.
Kati ya sura hizo, saba walikuwa mawaziri na watano walikuwa ni manaibu waziri, ambao Dk Magufuli amewaamini na sasa watakuwa mawaziri kamili, ambao wataungana naye kuunda Serikali ya Awamu ya Tano.
Mawaziri 7 wa JK warudishwa George Simbachawene ambaye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini sasa anakuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora, William Lukuvi amebaki Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Harrison Mwakyembe kutoka Ushirikiano wa Afrika Mashariki na sasa anakuwa Waziri wa Katiba na Sheria.
Mwingine ni Profesa Makame Mbarawa ametoka Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia sasa anakuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jenista Mhagama ametoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge na sasa ataongoza Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu na Dk Hussein Mwinyi aliyebakizwa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Mwingine ni Profesa Sospeter Muhongo.
Wakati huo, aliteuliwa na Rais kuwa mbunge, lakini safari hii ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini. Manaibu waziri 5 wa JK wapanda Manaibu wa JK waliopandishwa na Magufuli ni January Makamba anakuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu (Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto), Charles Mwijage (Viwanda, Biashara na Uwekezaji), Mwigulu Nchemba (Kilimo, Mifugo na Uvuvi) na Angela Kairuki (Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora) na Charles Kitwanga (Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mawaziri waliotupwa nje ambao ni wabunge ambao wameshinda ubunge, lakini hawakurudi kwenye Baraza la Mawaziri ni Dk Mary Nagu aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi Rais, Mahusiano na Uratibu, Profesa Jumanne Maghembe (Maji), Dk Shukuru Kawambwa (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Hawa Ghasia (Tamisemi), Sophia Simba (Jinsia, Wanawake na Watoto), Saada Mkuya Salum (Fedha) na George Mkuchika (Utawala Bora).
Manaibu waliotupwa nje ambao ni wabunge, ni Stephen Masele ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Charles Tizeba (Uchukuzi), Greyson Lwenge (Ujenzi), Janet Mbena (Viwanda na Biashara), Juma Nkamia (Habari) na Mahmoud Mgimwa (Maliasili na Utalii).
Mawaziri na manaibu walioshindwa kwenye uchaguzi Mawaziri wa JK walioshindwa Uchaguzi Mkuu na hawakufikiriwa tena na Magufuli ni Stephen Wassira (Kilimo, Chakula na Ushirika), Christopher Chizza (Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk Fenella Mukangara (Habari), Godfrey Zambi (Naibu-Kilimo), Aggrey Mwanry (Naibu-Tamisemi), Anne Kilango (Naibu-Elimu) na Dk Steven Kebwe (Naibu-Afya).
Mawaziri walioteuliwa na JK waliosahauliwa na JPM ni Dk Rose Migiro (Sheria na Katiba) yeye aliteuliwa kuwa mbunge na JK na safari hii hakugombea tena ubunge. Mawaziri wa JK walioshindwa kwenye kura za maoni Gaudetia Kabaka (Kazi na Ajira), Dk Bilinith Mahenge (Mazingira), Dk Seif Idd (Afya), Dk Titus Kamani (Uvuvi na Mifugo), Mathias Chikawe (Mambo ya Ndani), Adamu Malima (Naibu-Fedha), Kaika Telele (Naibu-Mifugo na Uvuvi), Amos Makalla (Naibu-Maji), Dk Abdallah Juma Abdallah (Naibu-Afrika Mashariki), Mahadhi Juma Maalim (Naibu Mambo ya Nje), Pereira Ame Silima (Naibu Mambo ya Ndani) na Pindi Chana (Naibu-Wanawake).
Mawaziri na manaibu wa JK ambao safari hii hawakugombea ubunge ni Mizengo Pinda (Waziri Mkuu), Bernard Membe (Mambo ya Nje), Profesa Mark Mwandosha (Kazi Maalumu), Samuel Sitta (Uchukuzi), Dk Makongoro Mahanga aliyehamia Chadema. Mawaziri wa JK ambao walifariki dunia ni aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda na Celina Kombani (Utumishi).
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment