Image
Image

Hii ndio kauli ya Kubenea aliyoitoa baada ya maafisa polisi kumkamata leo.

Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es salaam umezidi kuchukua vichwa vya habari baada ya kuahirishwa mara kadhaa na hata mara ya mwisho kuibuka kwa vurugu ambazo zilipelekea baadhi ya Wabunge wa Chadema na Madiwani wake kufikishwa mahakamani na baadae kuachiliwa kwa dhamana.
March 10 2016 Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), Saed Kubenea amehitajika polisi kwa tuhuma za kuhusika na vurugu  wakati uchaguzi huo ulipoahirishwa February 27 2016. Saed Kubenea ameelezea kuhusiana na wito huo wa polisi kwa ajili ya kujibu tuhuma hizo na amesimulia ilivyokuwa….
’Nimefuatwa na askari kama sita wakiniambia kwamba niko chini ya ulinzi ninahitajika makao makuu ya polisi Dar es salam nikahoji kosa langu ni nini? wakasema nikajibu tuhuma juu ya vurugu zilizotokea katika uchaguzi wa Meya wa Dar es salaam‘:-Saed Kubenea
Pia ameeleza kwamba hapo awali wakati tukio linatokea yeye hakuwa kwenye orodha ya washitakiwa kwa hiyo anakwenda kuwasikiliza na kama atapelekwa mahakamani anaamini haki itatendeka, Kubenea ameeleza..
’ninachokumbuka mimi nilifika makao makuu polisi kuwasilisha malalamiko juu ya amri iliyotolewa kwamba uchaguzi ule uzuiliwe, niliwathibitishia polisi kwamba amri ile ilikuwa haramu na ilikuwa imeexipire kwa hiyo ni lazima wachukue hatua za kisheria dhidi ya wahusika, na SP Ndalama ambaye ni mkuu wa upelelezi wa mkoa wa kipolisi  Ilala alikuwepo na alinipa orodha ya watu wanaotakiwa mimi jina langu halikuwemo‘:-Saed Kubenea
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment