Image
Image

CHAD kupiga kura kumchagua rais wao Leo.



Wananchi wa chad  leo wanapiga kura kumchagua rais wa nchi hiyo na mwelekeo unaonesha kuwa, rais wa sasa Idriss Deby,anapewa nafasi kubwa ya kurejea madarakani.
Rais Deby,ambaye aliingia madarakani kwenye mapinduzi ya kijeshi miaka 26 iliyopita, anakabiliwa na ushindani kutoka kwa wagombea 12, lakini anatarajiwa kushinda kwa awamu nyingine.
Katika wiki za hivi karibuni  maandamano yalipigwa marufuku  na baadhi ya wapinzani wa serikali kukamatwa.
Alhamisi  iliyopita  polisi walilazimika kutumia risasi za moto  na mabomu ya machozi kuwatawanya  mamia ya waandamanaji baada ya waendesha mashitaka kutaka  wanaharakati watano wanaoipinga serikali wafungwe jela miezi sita.
Mwaka 2011 wapinzani walisusia uchaguzi mkuu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment