Image
Image

Al-Shabab yauwa wanajeshi wa Ethiopia.

Kundi  la  kijihadi la  al-Shabaab limeshambulia kituo  cha jeshi  la  Umoja  wa  Afrika  nchini  Somalia, na  kuwauwa kiasi  ya  wanajeshi  30 wa Ethiopia. Maafisa  walisema wanamgambo  hao  waliripua  bomu  lililokuwa  katika  gari katika   lango  la  kituo  hicho katika  jimbo  la  Hiran, kabla ya  kujaribu  kukivamia. Watu  walioshuhudia  waliripoti kusikia   mripuko  mkubwa  uliofuatiwa  na  mapigano  ya risasi  muda  mfupi  kabla  ya  alfajiri. Milio  ya  risasi iliendelea   kusikika kwa  takriban  saa moja baada  ya mripuko kusikika. Pande  hizo  mbili zimetoa taarifa zinazokinzana juu  ya 
mapigano  hayo. Maafisa  wa Ethiopia  wanadai kwamba  shambulio  hilo lilizuiwa na kwamba  wanajeshi  wao  wamewauwa   zaidi   ya wanamgambo 100  wa  al-Shabaab. Kundi  hilo  la  al-Shabaab  lenye mafungamano na  al-Qaeda, limedai kwamba  limepoteza  wapiganaji  16.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment