Image
Image

Ulimwengu amvaa JK mchakato wa katiba mpya ya Tanzania*Asema anafaa kushitakiwa.

Mwanazuoni Mkongwe na Mwandishi wa Habari nguli nchini Tanzania  Jenerali Ulimwengu amesema Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete anapaswa kushtakiwa kama viongozi wengine walioisababishia hasara Serikali ya Tanzania wakati wa mchakato wa upatikanaji Katiba Mpya.

Akizungumza katika tamasha la Nane la Kigoda cha Mwalimu Nyerere leo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ulimwengu amesema fedha nyingi zimepotea wakati wa kuunda Katiba Mpya ambayo haikupatikana hadi hivi leo.
Hata hivyo, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo, amesema badala ya kumlaumu mtu mmoja mmoja, mjadala mpana wa kitaifa unahitajika kujua kilichosababisha Taifa kukosa Katiba Mpya.
“Hakuna anayeandika ni wapi tulipokwama, tunalaumu na kumjadili mtu. Wengine wanasema katiba imekwamishwa na watu wachache…tunapaswa kuwa na mjadala wa kina kujua ni wapi tulipokwama,” amesema Mkapa.
Akiwasilisha mada, Mkapa amesema si kwamba Mwalimu Nyerere hakupenda kampuni binafsi zije kuwekeza nchini bali alipenda biashara na uwekezaji ufanyike kwa haki, usawa na kuchangia maendeleo ya nchi.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment