Waziri mkuu wa Ufaransa Manuel Valls amesema leo kwamba nchi hiyo inafanya kila inaloweza kuzuwia mashambulizi ya kigaidi lakini yatakuwapo mengi.
Aliyasema hayo kufuatia kile maafisa nchini Ufaransa walichosema kwamba mtu aliyefanya shambulio baya la mauaji ya watu wawili alikula kiapo cha utii kwa kundi la kigaidi la Dola la Kiislamu.
Larossi Abballa mwenye umri wa miaka 25 alimchoma kisu afisa wa polisi hadi kufa katika kitongoji cha jiji la Paris usiku wa Jumatatu, kabla ya kumuua mke wa afisa huyo nyumbani kwao. Abballa binafsi aliuwawa baadaye kufuatia mapambano ya masaa matatu na polisi.
Jana Jumanne, maafisa walisema kwamba Abballa alikula kiapo mara kadhaa kwa kundi la Dola la Kiislamu na kiongozi wake, Abu Bakr al-Baghdadi katika video ya dakika 13 aliyoichukua mwenyewe nyumbani kwa wahanga.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment