Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. SALIM AHMED SALIM ametoa wito kwa vijana nchini kujua historia ya nchi na kudumisha ushirikiano na nchi nyingine kwa maendeleo ya taifa na AFRIKA kwa ujumla.
Dkt. SALIM amesema hayo jijini DSM katika hafla ya kutunukiwa MEDALI YA URAFIKI na serikali ya CUBA, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya nchi hiyo.
Kwa upande wake Balozi wa CUBA hapa nchini JORGE LOPEZ TORMO amesema nchi hiyo inatambua mchango wa Dkt. SALIM kwa aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo CHE GUEVARA.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi na mabalozi wa nchi mbalimbali, huku mgeni rasmi akiwa ni Rais wa awamu ya pili mzee ALI HASSAN MWINYI.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment