Ndege
ndefu zaidi duniani - Airlander 10 - imeharibika baada ya kuanguka
ikitua kwenye safari yake ya pili ya kufanyiwa majaribio.
Ndege hiyo
ya urefu wa 302ft (92m) - ambayo kwa kiasi fulani ni ndege na pia kwa
kiasi fulani puto - iliharibika ikiwa katika uwanja wa Cardington,
Bedfordshire nchini Uingereza.
Ndege hiyo ya thamani ya £25m
imeharibika eneo wanamoketi marubani baada ya kuangika kwa 'pua' mwendo
wa saa tano saa za Uingereza.
Msemaji wa HAV, kampuni iliyounda ndege hiyo, amesema marubani na wahudumu wengine wote wako salama.
Kampuni
hiyo imekanusha madai kwamba waya uliokuwa umening'inia kutoka kwenye
ndege hiyo ulikwama kwenye kigingi cha nyaya za simu na kusababisha
ajali hiyo.
Ndege hiyo ilifanya safari yake ya kwanza 17 Agosti.
Airlander 10 kwa takwimu
44,100 lbs (20,000kg): Uzani wa ndege hiyo
20,000ft (6,100m): Umbali ambao inaweza kupaa juu angani
80 knots (148km/h): Kasi yake ya juu zaidi
Siku 5: Muda ambao inaweza kukaa angani
22,050 lbs (10,000kg): Uzani ambao inaweza kubeba
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)



0 comments:
Post a Comment