Aliyewahi kuwa Rais wa Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe amefariki dunia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Akithibitisha
kutokea kwa kifo hicho Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Mh. Mohamed Abood amesema kuwa bado haijafahamika
kilichosababisha kifo chake mara moja, isipokuwa huenda ikawa
kimesababishwa na maradhi yatokanayo na umri.
"Ni ngumu kusema sababu za kifo lakini pengine ni uzee, maana umri wake ulikuwa umekwenda"amesema Abood.
Amesema
taarifa rasmi ya serikali itatolewa baadaye na kuwataka wazanzibar
wakiwemo ndugu jamaa na viongozi mbalimbai kuwa wavumilivu katika
kipindi hiki kigumu cha majonzi.
Aidha Maziko yatafanyika kesho visiwani Zanziabr baada ya mwili wake kusafirishwa kutoka Dar es salaam, leo. Historia
Aboud
Jumbe Mwinyi alizaliwa Tarehe 14 mwezi Juni mwaka 1920, na amefariki
leo tarehe 14 Agosti mwaka 2016 akiwa na umri wa miaka 96.
Wakati wa
uhai wake alishika nyazifa mbalimbali ikiwemo ya urais wa awamu ya pili
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamu Mwenyekiti wa
CCM, Zanzibar.
Alikuwa Rais wa Zanzibar kuanzia April 11 mwaka 1972
hadi tarehe 30 Januari mwaka 1984 akichukua nafasi ya Rais wa Kwanza wa
nchi hiyo Abeid Karume aliyeuawa April 7, 1972.
Alishika nafasi hiyo
ya urais kwa kuhaguliwa na Baraza la Mapinduzi wakati huo likiwa chini
ya chama cha ASP kabla hakijaungana na TANU na kuzaa Chama Cha Mapinduzi
mwaka 1977.
Mwaka 1979, Jumbe alisukuma mabadiliko ya Katiba yaliyotenganisha majukumu kati ya Baraza la Mapinduzi na Baraza la Wawakilishi.
Mabadiliko
mengine yaliyofanyika katika katiba ni kuwezesha wananchi kumchagua
Rais kupitia uchaguzi wa kidemokrasia badala ya utaratibu uliokuwepo
ambapo Rais alikuwa akichaguliwa na Baraza la Mapinduzi.
Jumbe atakumbukwa kwa kuwa kiongozi mwenye msimamo thabiti katika kusimamia maamuzi yake na serikali, wakati wa uhai wake.
Home
News
Slider
TANZIA:Aliyewahi kuwa Rais wa Zanzibar Aboud Jumbe afariki dunia jijini Dar es Salaam.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment