Image
Image

EXCLUSIVE: TFF YAWAPONGEZA WASHINDI WA TUZO ZA MICHEZO 2013

Utoaji wa Tuzo za (EJAT) 2013.
Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania (TFF) limewapongeza waandishi wa habari watatu wa habari za michezo kwa kushinda tuzo ya umahiri wa uandishi wa Habari (EJAT) inayotolewa na Baraza la Habari Nchini Tanzania (MCT).

TFF inawapongeza kwa ushindi huo uliotokana na makala zao ambazo zina mchango mkubwa katika maendeleo ya mpira wa miguu, na kutoa wito kwa waandishi zadi kutumia changamoto hiyo kushiriki katika kukuza michezo na hatimaye kufichua maovu yanayojitokeza kama vile Rushwa kwenye sekta hiyo hususani mpira wa miguu.

Hata hivyo waandishi waandishi waliokuwa wameshinda katika Kategori ya Michezo na utamaduni alikuwa ni Abdul Mohammed wa Mwananchi, Pamoja na Abdallah Majura wa radio ABM kwa upande wa radio.

Aidha katika hatua nyingine TFF imeipongeza timu ya Azamu FC kwa kufanikiwa kusonga mbele kwenye raundi ya pili ya michuano ya kombe la shirikisho baada ya kuitoa timu ya Barrack Young Controllers  ya Liberia katika mchezo wa mwisho mwa wiki.

Azam FC
Azam sasa itapambana na timu ya FAR Rabat inayo milikiwa na jeshi la morogoro.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment