Mapema leo akikabidhi hundi ya shilingi milioni tatu kwa katibu mtendaji wa MCT,Kajubi Mukajanga,mwenyekiti na afisa mtendaji mkuu wa Excecutive Solutions,Aggrey Mareale amesema kampuni yake imeamua tena kudhamini tuzo hizo kwa kuthamini na kutambua kazi kubwa inayofanywa na Waandishi wa Habari.
Mareale amesema kampuni yake itaendelea kudhamini vipengele vya uchumi na biashara,afya,michezo,mawasiliano na teknologia,elimu,na mpiga picha bora.
Hata hivyo amelipongeza baraza la habari Tanzania kwa kuandaa tuzo hizo huku akisema hicho ni kichochea mojawapo kwa waandishi wa habari kuongeza bidii katika kazi na kuzingatia maadili na taaluma ya kazi hiyo.
![]() |
Kajubi Mukajanga - katibu mtendaji wa MCT |
Akipokea hundi hiyo Mukanjanga ameipongeza Executive Solutions kwa kuthamini kazi za waandishi wa Habari na kushiriki katika tuzo hizo kwa mwaka wa pili mfululizo.
Aidha Tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika kesho ijumaa katika ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Raisi wa Zanzibar Dk.Ally Mohammed Shein.



0 comments:
Post a Comment