Image
Image

EXCLUSIVE: TIMU YA TAIFA UFARANSA KUKUTANA NA UBELGIJI KWENYE MECHI YA KIRAFIKI AGOSTI 14.

Timu ya taifa ya Ufaransa les Blues watakutana katika mechi ya kirafiki na ubelgiji ifikapo Agosti 14 jijini Brussels, shirika la mpira wa miguu nchini Ufaransa FFF limethibitisha

Vijana wa timu ya taifa ya Ufaransa ya mpira wa miguu wakiwa uwanjani wakipasha kabla ya mechi.


























Kabla ya mechi hiyo, vijana wa Didier Deschamps watakuwa katika mzunguuko Amerika Kusini mwezi Juni kukiwa na mpango wa kucheza mechi mbili za kirafiki, tarehe 5 na Uruguay mjini Montevideo, na tarehe 9 Juni jijini Alegro na Brazil.

Baada ya hapo les blues wataendelea na mechi za mchuano wa kufuzu kombe la dunia la mwaka 2014 nchini Brazil kwa kumenyana na Georgia tarehe 6 septemba kabla ya kupepetana na Belarusi tarehe 10 mwezi Septemba.

Ufaransa na Ubelgiji zimekutana mara 51, mara ya mwisho ilikuwa Novemba 15 mwaka 2011 kwenye uwanja wa Stade de France katika mechi ya kitafiki ambapo timu hizo zilitoka sare ya kutofungana yani sufuri kwa sufuri.

 Ubelgiji kwa sasa inawachezaji wazoefu kama vile Hasard, Witsel, Fellaini, Defour, Kompany na wengine kibao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment