Image
Image

EXCLUSIVE: TPSF YAUNGA MKONO MKAKATI ULIOTANGAZWA NA PINDA.


Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imesema inaunga mkono mkakati uliotangazwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wa serikali kutumia mtindo mpya wa utendaji kazi ambao uliwahi kutumiwa na nchi ya Malaysia na kuwapatia mafanikio makubwa kiuchumi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi  ya Sekta Binafsi Tanzania, Godfrey Simbeye amewaambia Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam, baada ya kukamilika kikao cha wanachama wa TPSF wa mikoa ya Dar es salaam,Lindi, Mtwara na Zanzibar, ambacho kilikuwa kinafanya maandalizi ya uchaguzi wa kupata bodi mpya.
Godfrey Simbeye - Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania
Amesema Serikali imeamua kufanya mabadiliko ya utendaji kazi kwa kutumia mtindo huo mpya ujulikanao "President's Delivery Bureau (PDB) ambao uliwahi kutumiwa na nchi ya Malaysia unaojulikana kama Perfomance Management and Delivery Bureau.

Naye Mjumbe wa bodi ya TPSF, Arnold Kileo ambaye pia aliwahi kuwa mwenyekiti wa taasisi hiyo, amesema mtindo huo mpya utaleta tija kubwa kiuchumi na ambao unaendeshwa na sekta binafsi.
Arnold Kileo - Mjumbe wa Bodi ya TPSF
TPSF imeanza mchakato wa kupata bodi mpya ifikapo juni mwaka huu, baada ya kufanya uchaguzi ambao utasaidia wafanyabiashara kuwa na sauti moja ya kuleta mabadiliko na uchumi wa nchi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment