![]() |
| DK. HARRISON MWAKYEMBE |
Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa Taswa Juma Pinto, ambapo amesema lengo la kumwalika Mwakyembe nikwaajili ya kuweza kutoa zawadi za vikombe na medali kwa waandishi watakao ibuka washindi siku hiyo pamoja na kuzungumza na washiriki wa bonanza hilo.
Bonanza la mwaka huu litakuwa bonanza la tofauti na miaka iliyopita, kwa kuwa litashirikisha sekta mbali mbali katika tasnia hiyo ya habari, Ikiwemo afya, uchumi, siasa, Pamoja na michezo, ili kufanya kila mmoja afurahie kutokana na bonanza hilo kuwa linafanyika Mara moja kwa mwaka kwa hiyo ni nafasi ya kipekee.
Amesema bonanza la mwaka huu litahusisha wadau 1500 kutoka vyombo mbali mbali vya habari nchini, huku kukiwa na burudani ya muziki, ambapo siku ya Alhamisi Aprili 4,2013
saa tano asubuhi kutakuwa na mkutano na wanahabari mgahawa wa City
Sports Lounge, Posta Dar es Salaam ambao ni maalum kutangaza makundi
yatakayotumbuiza kwenye Media Day na tunatarajia makundi hayo nayo
yatakuwepo kwenye mkutano huo.
Hata hivyo ameviomba vyombo vya habari ambavyo havijathibitisha ushiriki wao kwa njia ya
maandishi vifanye hivyo kama vilivyoagizwa kwenye barua zao za mialiko,
vinginevyo ushiriki wao hautathaminika.
Aidha bonanza
hilo litafanyika Jumamosi wiki hii viwanja vya Sigara, Chang’ombe, Dar
es Salaam kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa moja usiku likidhaminiwa na
na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).


0 comments:
Post a Comment