NAHODHA na Beki wa Everton, Phil Neville,
ataondoka Klabu hiyo mwishoni mwa Msimu huu.
Mchezaji huyo wa zamani wa England na Manchester
United, mwenye Miaka 36, Mkataba wake na Everton unamalizika Juni 2013 na
hataongeza Mkataba huo lakini hajatangaza kustaafu.
![]() |
| Phil Neville |
Phil Neville ametamka: “Nataka kuendelea kucheza
Soka katika ngazi ya juu kwa muda mrefu zaidi kadri inavyowezekana na nitakaa
nitafakari nini cha kufanya.”
Msimu huu, Phil Neville, ameichezea Everton Mechi
25 ikiwa ni sehemu ya Jumla Mechi 303 alizoichezea Klabu hiyo na kwenye Ligi
Kuu amecheza zaidi ya Mechi 500 zikiwemo zile alipokuwa Man United.


0 comments:
Post a Comment