Anasema yeye ni mhudumu pekee katika zahanati hiyo,
inayopatikana katika kata ya Kipugira wilaya ya Rufiji, kutokana na hali
hiyo hujikuta katika hali ngumu katika kumzalisha mama mjamzito hasa pale taa
yake ya chemli inapoisha mafuta.
Victor anaelezea hali ngumu anayokumbana nayo pale mjamzito
anapomfikia, na akiwa hana mafuta ya taa kwenye chemlii, ambapo
hulazimika kutumia tochi yake ya nyumbani ili kuhakikisha anamsaidia
mjamzito.
“Niko peke yangu kwa hiyo nalazimika kumuomba mlinzi
msaada wa kumlikiwa ili angalau nifanye kazi yangu vizuri, hali ambayo
kimaadili si sahihi ila nakosa namna ya kufanya” analalamika Victor.
Kwa niaba ya Kalulunga.


0 comments:
Post a Comment