Kamishna wa kamati ya amani na usalama ya
Umoja wa Afrika Bw, Ramtane Lamamra jana alisema mjini Addis Ababa kuwa umoja
huo unatarajia kuongeza ushirikiano na China katika juhudi za kulinda amani na
usalama barani Afrika.
Bw. Lamamra alisema Umoja wa Afrika unatumai
kusaini makubaliano halisi na China, ili kuongeza ushirikiano kati ya pande
hizo mbili katika juhudi za kulinda amani na usalama barani Afrika.
Bw.Lamamra alisema, anaona China inaweza
kuusaidia Umoja wa Afrika kutekeleza operesheni ya kulinda amani, na pia
inaweza kuusaidia umoja huo kufundisha majeshi, na kuyapatia zana za kijeshi.


0 comments:
Post a Comment