 |
| Wabunge wakitafakari Bajeti wakati ikisomwa leo. |
Serikali imetangaza marekebisho ya sheria za kodi
kadhaa ikiwemo ya mapato na ushuru ambapo, kodi za bidhaa mbalimbali
zinazozalishwa hapa nchini na kutoka nje kama vinywaji, sigara, nishati ya mafuta
na magari zimepanda kwa viwango tofauti.
 |
Dk,William Mgimwa
Akiwasilisha bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha
2013/2014 Bungeni leo, Waziri wa Fedha Dk,William Mgimwa amesema lengo ni
kuongeza mapato ya ndani na kupunguza uingizaji wa magari chakavu na kulinda
viwanda vya ndani vinavyozalisha samani.
|
Waziri Mgimwa amesema kodi ya mafuta ya Dizeli
imepanda kwa kiasi cha shilingi mbili kwa lita kwa kutambua kwamba magari
makubwa na mitambo mbalimbali inatumia mafuta hayo katika shughuli mbalimbali.
 |
| James Mbatia ( kushoto) na Waziri mkuu mizengo Pinda wakijadiliana mambo kadhaa wakati waziri mgimwa akiendelea kusoma bajeti kwa mwaka 2013/ 2014 - Bungeni mjini dodoma leo. |
Aidha, kodi ya Mafuta ya Petroli imepanda kutoka
shilingi 300 hadi 400 kwa lita huku, kodi ya mafuta ya taa ikibaki bila
ongezeko lolote.
 |
| James Mbatia ( kushoto) na Waziri mkuu mizengo Pinda wakijadiliana jambo wakati bajeti ikiendelea kusomwa leo, wengine wanao onekana ni baadhi ya wabunge wakifuatilia kwa umakini. |
 |
| Mh. Bernad Membe( kulia) akionekana kuteta jambo. |
Akizungumza kodi ya mapato ya ajira, Waziri Mgimwa
amesema Serikali imepunguza kodi hiyo kutoka asilimia 14 mpaka 13 hatua ambayo
itakuwa nafuu kwa wafanyakazi.
 |
| Mh. Mbowe (kushoto) na john mnyika (katikati) zitto kambwe mwishoni, wakonekana kutafakari bajeti kwa dizaini tofauti Bungeni Mjini Dodoma Leo |
Katika bajeti
hiyo ya mwaka wa fedha 2013/14,Serikali inakusudia kukusanya shilingi trilioni
18.2 kutoka vyanzo vyake vya ndani nje ikilinganishwa na bajeti ya mwaka
iliyopita na kwamba na bajeti hiyo inazingatia vipaumbele vilivyoanishwa katika
mpango wa maendeleo wa mwaka 2013/2014
na mfumo mpya wa utekelezaji wa vipaumbele vyenye matokeo makubwa na ya haraka.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment