Msafara wa timu ya taifa ya Ivory Coast "The
Elephants" watu 80 wakiwemo wachezaji 27 unatarajiwa kuwasili nchini usiku
huu kwa ndege maalum kwa ajili ya mechi ya marudiano dhidi ya Timu ya soka ya Tanzania Taifa Stars
kwa jili ya kusaka tiketi ya kushiriki kwenye fainali ya Kombe la dunia mwakani
nchini Brazil.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF) Boniface Wambura,kikosi hicho cha Ivory Coast ambacho kitawasili bila ya nyota wake Didier Drogba kitafikia kwenye hoteli ya Bahari Beach iliyopo nje Kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na kitaondoka saa chache baada ya mechi hiyo ya Jumapili.
 |
Boniface Wambura
Mchezo huo
utakaochezeshwa na Mwamuzi kutoka Algeria utafanyika kwenye Uwanja wa
Taifa Jijini Dar es Salaam siku ya Jumapili saa tisa alasiri ambapo tiketi
zitaanza kuuzwa keshokutwa ambapo kiingili cha chini kitakuwa ni shilingi 5000
kwa viti vya rangi ya kijani.
Baadhi ya wachezaji nyota wanaounda timu hiyo ni pamoja na Mwanasoka bora wa
Afrika Yaya Toure,Tiote Cheik,Arouna Kone,Salomon Kalou,Seydou Doumbia na Sio
Giovanni.
Wakati Ivory Coast ambayo inaongoza kwenye kundi C wanawasili leo,Taifa Stars ambaye imeweka kambi kwenye hoteli ya Tansoma inaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa chini ya Kocha Mkuu Kim Poulsen kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo.
Wakati huo huo makocha wa timu zote mbili Taifa Stars na Ivory Coast watakutana na Waandishi wa Habari Jumamosi kwenye makao makuu wa TFF
|
|
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment