Image
Image

EXCLUSIVE: JESHI LA POLISI KANDA MAALUMU DAR ES SALAAM LASEMA LIMEJIPANGA VEMA KUIMARISHA ULINZI DHIDI YA MECHI YA IVORY COAST NA TAIFA STARS.


Wakati Ivory Coast wakiwasili nchini Jeshi la polisi kanda maalum Dar es Salaam limesema limejipanga katika kuimarisha ulinzi na usalama katika mechi kati ya taifa stars na ivory cost inatarajiwa kufanyika siku ya jumapili katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.

Kamishna wa polisi kanda maalum ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya usalama wa uwanja huo amesema ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia na silaha zikiwemo zile za moto au visu na magari yote yataegeshwa nje ya uwanja huku magari ya kazi maalum na viongozi tu ndiyo yataruhusiwa kuingia uwanjani hapo.
Suleiman kova - Kamishna wa jeshi la polisi  kanda maalum DSM.

Aidha jeshi hilo limewatahadharisha mashabiki kuzingatia sheria na kufuata taratibu zinazokubalika uwanjani hapo kwa kuwa tayari hatua za kiusalama za kubaini wakorofi zimechukuliwa baada ya kuweka kamera za usalama kila kona ya uwanja huo wa taifa.




Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment