Image
Image

IVORY COAST YAWASILI NCHINI KWA MBWEMBWE DHIDI YA MCHEZO WAKE NA TAIFA STARS UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM.


Timu ya soka ya Ivory Coast imewasili nchini jana usiku kwa tayari kwa mchezo dhidi Taifa Stars kwa ajili ya kusaka tiketi ya kushiriki kwenye fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil Mwakani.

Timu hiyo imewasili ikiwa ni nyota wake kadhaa akiwemo kiungo wa Manchester City Yaya Toure,Gervihno wa Arsenal,Tiote wa New Castle,Solomon Kalou anayesakata soka nchini Ufaransa na Arouna Kone.

Timu hiyo imewasili bila nyota wake Didier Drogba anayechezea Galatasaray ya Uturuki.

Wakati Timu hiyo Stars ambayo imeweka kambi kwenye hoteli ya Tansoma imendelea na mazoezi kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam kujiandaa na mchezo huo utakaofanyika Jumapili.

Wakati huo huo makocha wa timu zote mbili watakutana na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya shirikisho la soka nchini (TFF) kwa ajili ya kuzungumzia jinsi walivyojiandaa kwa mechi hiyo.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment