Image
Image

EXCLUSIVE: SERIKALI KUZIRUDISHA TMU ZA SIMBA YANGA NA FALCONS KUSHIRIKI MICHUANO KOMBE LA KAGAME SUDANI.


Na. Kuringe Mongi, Dodoma.

Hatimaye Serikali imetoa msimamo mpya wa kuziruhusu timu za Yanga Simba na Super Falcons ya Zanzibar kushiriki kwenye michuano ya Kombe la Kagame nchini Sudan baada ya kuhakikishiwa na Serikali ya nchi hiyo kwamba itatoa ulinzi wa kutosha kwa ya timu za Tanzania.

Naibu Waziri Habari  Vijana Utamaduni na Michezo Amos Makalla akizungumza na Waandishi wa Habari Mkoani Dodoma amesema kwamba wameandikiwa barua na serikali ya Sudan ikiwahakikishia kwamba timu za Tanzania zitapewa ulinzi mkubwa zisiweze kudhurika na  machafuko yanayoendelea Sudan.
Amos Makalla - Naibu waziri wa Habari Vijana Utamaduni na michezo.
Amesema licha ya serikali kuja na msimamo mpya bado ni jukumu la timu hizo kuamua kwenda au kutokwenda Sudan kwa ajili ya Michuano hiyo ya Afrika Mashariki na Kati inayotarajiwa kuanza juni 18 mwaka huu.

Tamko hilo na serikali limekuja siku chache baada ya Katibu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Mkenya Nicholas Musonye  kutoa tishio la kuzichukulia hatua kali dhidi ya timu hizo za Tanzania endapo hazitakwenda kushiriki kwenye michuano hiyo mjini Khatoum.

Yanga wamepangwa Kundi C katika michuano hiyo pamoja na Ports ya Djibouti, Express ya Uganda na Vital 'O' ya Burundi, wakati wapinzani wao wa jadi, Simba SC wamepangwa Kundi A pamoja na wenyeji El-Mereikh, Elman  ya Somalia na APR ya Rwanda.

Awali  Serikali  ilitoa tamko la kuzuia klabu za Tanzania kutokwenda Sudan kutokana na machafuko yanayoendelea nchini humo.




Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment