Image
Image

EXCLUSIVE: PINDA ATOA WITO KWA WABUNGE KUPAMBANA NA RUSHWA.


Na .Kuringe Mongi, Dodoma.

Waziri mkuu Bw. Mizengo Pinda ametoa wito kwa wabunge kupambana na rushwa (APNAC) tawi la Tanzania, kuingalia upya sheria ya rushwa na kuifanyia marekebisho, ili Taasisi ya kudhibiti na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) iweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu.


Waziri Mkuu ameitoa rai hiyo mjini Dodoma, wakati alipokuwa akifungua mkutano wa (APNAC) tawi la Tanzania, na kuweka wazi juu ya malalamiko yanayohusu Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuwa na mamlaka ya mwisho ya kesi za rushwa nchini.

Aidha, Waziri Mkuu amewataka wabunge hao ambao ni wanachama wa (APNAC) kuipinga rushwa kwa nguvu zote, kwani hata vitabu vitakatifu, vimekuwa vikionya juu ya rushwa.
Naye, Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Bibi Anne Makinda akimkaribisha waziri mkuu kufungua mkutano huo, hakusita kuwataka wabunge kuwa na nia ya dhati kukataa kuchukua rushwa, kama kweli wanataka kuisimamia serikali.
Anne Makinda - Spika wa Bunge la Tanzania.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment