Image
Image

EXCLUSIVE: TARATIBU ZA MAZISHI YA MSANII LANGA BHADO ZINAENDELEA KUFANYIKA NYUMBANI KWA MSANII HUYO MTAA WA LUNDI MIKOCHENI JIJINI DAR ES SALAAM.


Msanii wa maarufu wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania wa  miondoka ya Hip Hop Langa Tottym Kileo maarufu kama Langa aliyefariki jana kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili anatarajiwa kuzikwa Jumatatu kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Taratibu za mazishi zimekuwa zikiendelea kufanyika  nyumbani kwa msanii huyo mtaa wa Ludi Mikocheni Jijini Dar es Salaam ambako baadhi ya ndugu na jamaa  na wasanii wenzake walikukusanyika  kwa ajili ya kuomboleza msiba huo.
Marehemu Langa Tottym Kileo enzi za uhai wake.
Wakizungumzia jinsi walivyo pokea  kifo cha msanii huyo,  wasanii Kala Jeremiah na Mukhi Edwards wamesema kwamba ni pigo jingine kwenye tasni ya muziki wa hip hop nchini na kwamba kifo chake hakitasahaulika.
Kala Jeremiah - Mwanamuziki  wa Hip hop Tanzania
Langa alitambulika  kwenye mashindano yaliyofanyika mwaka 2004 ya Coca-Cola Pop Star yaliyofanyika Afrika Kusini kwa kujumuisha nchi tatu za Afrika Mashariki ambapo enzi za uhai wake mwanamuziki huyo alitamba na vibao kama Kiswanglishi,unanicha hoi.matawi ya juu akiwa na kundi maarufu la Wakilisha la jijini Dar es Salaam na nyimbo nyingine nyingi.

Langa alizaliwa desemba 23 mwaka 1985 na  amekutwa na umauti wakati akiwa anaumwa malaria wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa  muhimbili ambapo hapo ndipo ikawa safari yake ya mwisho kimuziki.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema Amen




Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment