Image
Image

EXCLUSIVE: MPOTO KUHAMASISHA USAFI WA VYOO.



Msanii maarufu wa mashairi nchini Mrisho Mpoto pamoja na kundi lake la Mpoto Theatre Gallery Limited, likiwa na jumla ya wasanii 28 anatarajiwa kuanza kampeni ya siku 45 ya uhamasishaji wa usafi wa vyoo,mazingira na mikono katika mikoa mitano ya Tanzania Bara juni 20.

Akizungumzia kampeni hiyo inayolenga nchi nzima ikianzia  mikoa ya Dodoma,Mara,Njombe,Rukwa na Tanga.

Mpoto,amewaambia waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam kuwa msanii wa vichekesho King Majuto atakuwemo pia katika kampeni hiyo yenye lengo la kutoa elimu kwa jamii hususani ya vijijini, namna wanavyoweza kuepuka maradhi hasa ya tumbo yatokanayo na matumizi yasiyo sahihi ya vyoo na kutonawa mikono kwa hatua stahiki.


Awali Afisa mazingira kutoka wizara ya afya na ustawi wa jamii,Mariamu Mahmoud,alisema,kampeni hiyo ni muendelezo wa kampenu ya kitaifa zinduliwa na Rais Jakaya Kikwete Juni 5 Mjini Moshi akati wa kilele cha siku ya usafi wa mazingira duniani.

Kwa Mujibu wa takwimu za kitaifa,asilimia 91 ya wananchi wa vijijini hawana elimu juu ya matumizi sahihi ya vyoo bora na unawaji stahiki wa mikono hali inayochangia vifo vitokanavyo na maradhi ya tumbo



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment