Image
Image

EXCLUSIVE: TATU AOMBA MSAADA KWA WASAMARIA WEMA AWEZE KUWEKEWA MIKONO BANDIA.

Tatu Juma
Msichana Tatu Juma, mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa jijijni dar es salaam ambae amekatwa mikono yake yote miwili kutokana na ajali ya gari anaomba msaada wa kifedha kutoka kwa wasamalia wema ili aweze kununua mikono bandia itakayomwezesha kujihudumia mahitaji yake ya msingi.


Tatu Juma ndivyo anavyoonekana hali yakuwa mikono yake ikiwa imekatika.
Akizungumza kwenye ofisi za channel ten ambako alifuatana na mlezi wake, binti huyu  Tatu ambae alimaliza kidato cha nne katika shule ya sekondari Kileo moshi mwaka 2010 na kupata ajali ya gari ya  daladala jijini dar es salaam mwaka  2012 ambapo alikatika mkono mmoja hapo hapo na mwingine walimalizia hospitali ya mifupa MOI kutokana na kupondeka kabisa.

Binti huyu anasema kutokana na ulemavu alioupata wa kupoteza mikono yake yote miwili hawezi hata  kufanya kitu chochote, hivyo kulazimu kutegemea ndugu zake wamsaidie.

Tatu Juma ( kulia)  akiwa na mlezi wake Hawa Msuya kwenye ofisi za Channel Ten. Amesema wamepata hospitali nchini afrika ya kusini ambayo wanaweza kumpatia mikono itakayomwezesha kujihudumia mambo ya msingi na kufanya vitu vidogo vidogo,  ambapo gharama za kikono peke yake ni sh million arobaini na tano, wakijumlisha nauli za watu wawili na gharama nyingine inafika sh million sitini fedha za kitanzania ambazo yeye na familia yake hawana uwezo wa kuzipata, hivyo amewaomba watanzania ambao wataguswa na tatizo lake kumsaidia. ili aweze kupata mikono hiyo ya bandia.
Kwa yeyote atakayeguswa na matatizo ya Tatu na kutaka kuchangia matibabu yake ya kupata mikono ya bandia anaweza kuwasiliana nae kwa namba ya simu 0713 466721, au 0767 768 785 au 0715 501 223, na anaishi jijini dar es salaam.




Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment