Image
Image

EXCLUSIVE: MKOANI SHINYANGA MAMIA WAJITOKEZA KWA WINGI KUMZIKA, MWANDISHI WA HABARI WA CHANNEL TEN CHARLES HILILA


Mamia ya wakazi wa mkoa wa Shinyanga jana wamejitokeza kwenye mazishi ya aliyekuwa mwakilishi wa kituo cha televisheni cha Channel Ten na Magic Fm mkoani humo, Marehemu Charles Hilila aliyefariki dunia usiku wa kuamkia June 19 mwaka huu katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga.
Marehemu Charles Hilila Enzi za Uhai Wake.
Marehemu Charles Hilila aliyezaliwa September 15 mwaka 1964, amezikwa jana katika kijiji cha Tinde mkoani Shinyanga ambapo katika ibada ya mazishi Padri Emmanuel Kakoro wa kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Shinyanga aliwakumbusha wanadamu kumrejea Mwenyezi mungu muda wote kutokana na mema anayowatendea.

Katika mazishi hayo kampuni ya Afrika Media Group, inayomiliki vituo vya televisheni vya Channel Ten, CTN, C2C, DTV na Radio Magic Fm iliwakilishwa na mwandishi wake wa mkoani Mwanza bw. Henry Kavirondo.

Nao baadhi ya waliomfahamu marehemu Charles Hilila wakati wa uhai wake wakiwemo wakazi na wanahabari wa mkoa wa Shinyanga walimuelezea kwa mtazamo tofauti.

Marehemu Charles Hilila ambaye tulimpenda lakini Mwenyezi Mungu amempenda zaidi ameacha mjane na watoto watatu.......

Mungu ailaze roho ya marehemu Charles Hilila mahala pema Amina.







Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment