Image
Image

BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI KUJADILI UZITO WA MIZIGO.


Bunge la Afrika mashariki linatarajiwa kujadili na kupitisha miswada miwili ya sheria ya kuwa na kiwango kimoja cha uzito wa mizigo na kuwa na kituo kimoja cha ukaguzi katika mipaka ya nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam, katibu wa wabunge wa Tanzania katika bunge hilo la Afrika Mashariki, bi. SHYROSE BHANJI, amesema kwa mara ya kwanza vikao vya bunge hilo vitaanza kuendeshwa kwenye makao makuu ya jumuiya hiyo jijini Arusha, Agosti mwaka huu ambapo miswada hiyo itajadiliwa na baadae marais wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo watatia saini ili kuwa sheria kamili.
SHYROSE BHANJI
Bi. Shyrose aliyekuwa ameongozana na mbunge  Abdullah Mwinyi wamesema faida ya miswada hiyo kwa nchi wanachama ni pamoja na kuwezesha nchi hizo kuwa na kiwango kimoja cha uzito wa mizigo barabarani ili kudhibiti uharibifu wa miundombinu hiyo pamoja na kuondoa urasimu na ucheleweshaji katika mipaka ya nchi hizo, hatua ambayo itaongeza kasi ya ukuaji wa biashara baina ya nchi wanachama.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment