Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi,
Profesa, ANNA TIBAIJUKA amewataka wananchi kuwa na tabia ya utaifa na uzalendo
hususan katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kufanikisha miradi hiyo
kwa wakati na kuchochea kasi ya maendeleo.
![]() |
| Prof Anna Tibaijuka |
Prof Tibaijuka ametoa rai hiyo jijini Dar es salaam
wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wa Makongo Juu katika manispaa ya
Kinondoni waliokutana kujadili juu ya mradi wa uboreshaji na uendelezaji wa
eneo hilo ili kupata ardhi kwa ajili ya huduma za jamii ambapo amewasisitizia
kuwa wakazi watakaoathirika na mradi huo,watalipwa fidia kwa mujibu wa sheria
na viwango vya soko na utakuwa mradi shirikishi.
Baadhi ya wakazi wa eneo hilo la makongo juu wakitoa
maelezo yao yametaka kujua mustakabali wao katika mpango huo wa uendelezaji
upya wa eneo hilo ikiwemo ujenzi wa viwanda vidogo,maeneo ya biashara na huduma
nyingine za jamii. Eneo hilo linakadiriwa kuwa na kaya


0 comments:
Post a Comment