Image
Image

ABRAMOVICH KUBEBA MIKOBA YA WAKONGWE ILI KUZALISHA WACHEZAJI WENYE VIPAJI.


Mmiliki wa klabu ya Chelsea Roman Abramovich akitimiza miaka kumi ya umiliki wake darajani na kupondwa na baadhi ya makocha kwa sera yake ya kutumia fedha nyingi kununua wachezaji nje ya England na kuwanyima wazawa nafasi ya kucheza, sasa bilionea huyo mwenye kiburi cha pesa amesema anahitaji kuona maendeleo makubwa katika kituo cha kulelea vipaji cha klabu hiyo (Chelesea Academy) ili kuijenga upya timu Hiyo.
Abramovich, kulia, akishangilia na  Frank Lampard, katikati, na John Terry, kushoto, mnamo mwaka  2005  
Terry enzi za ujana wake katika klabu ya  Chelsea career
Roman Abramovich anataka wachezaji vijana zaidi kutoka katika Akademi yake ya Chelsea.
Kwa mujibu wa mtandao Sportsmail.com ulioeinasa kauli ya bilionea huyo kuwa anahitaji kuzalisha wachezaji wa kwake siku zijazo ili kuwarithi wakongwe wa klabu hiyo.
Wapo wachezaji wakongwe kama vile  nahodha John Terry na Frank Lampard – ambao walisainishwa mwaka 2001 kutoka West Ham,
Ambapo hadi wakati huu wanaonekana kuwa ni nguzo muhimu ndani  ya klabu.

Nyota wa Chelsea Ryan Bertrand, akiwa na meneja wake Jose Mourinho katika mazoezi ya kujiandaa na msimu mpia.
Aidha  Abramovicha amedai anatakiwa kuzalisha wachezaji wapya kutoka katika Akademi yake na kuachana na hasara kubwa anayoipata  kwa kununua wachezaji wa bei kubwa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment