Image
Image

DK. SHEIN: SERIKALI YA ZANZIBAR INAWAKARIBISHA WAWEKEZAJI KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA UVUVI.


Munir Zakaria, Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amesema Serikali yake inawakaribisha wawekezaji kutoka nchini Uingereza kuwekeza katika sekta ya uvuvi wa bahari kuu, ili iweze kubadilisha maisha ya wananchi wengi wa visiwani humo.

Dk.Shein ametoa wito huo alipokutana na Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Bw.Mark Simmonds aliyemtembelea ofisini kwake Ikulu mjini Zanzibar.


Katika mazungumzo hayo ambayo pia yamehudhuriwa na Balozi wa uingereza hapa nchini Bibi Diana Melrose, Dk.Shein amesema jitihada za pamoja za kuimarisha ushirikiano katika biashara na uwekezaji zitasaidia kuongeza kasi ya uchumi hapa nchini.

Dk.Shein amemueleza Waziri huyo kuwa Serikali yake imedhamiria kukuza sekta ya uvuvi wa bahari kuu, ambayo hadi hivi sasa haijapata wawekezaji, na kuelezea matumaini yake kuwa wawekezaji kutoka Uingereza watachangamkia fursa hiyo kuwekeza visiwani hapa.

Aidha Dk.Shein ameishukuru Serikali ya Uingereza kwa misaada yake kwa Tanzania, ambayo pia inainufaisha Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wake, Waziri Mark Simmonds amesema dhamira ya Serikali ya uingereza ni kupanua maeneo mapya ya ushirikiano katika Nyanja za biashara na uwekezaji.

Waziri Simmonds amesema pamoja na Uingereza kuongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania, kuna umuhimu mkubwa kwa nchi hiyo kuimarisha zaidi uwekezaji na biashara kwa faida ya serikali na wananchi wa pande zote mbili.
Viongozi wengine waliohudhuria mazungumzo hayo ni pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais wa Zanzibar, Dk.Mwinyihaji Makame na Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Abdulhamid Yahya Mzee.

Katika kufanikisha utekelezaji wa mradi huo kwa haraka, serikali imeamua kuupa kipaumbele kwa kuuingiza katika mpango wake wa matokeo makubwa ya haraka sasa (Big Results Now), ambapo ujenzi wake utachukua miezi kumi na minane na kukamilika mwaka 2014, ambapo utakuwa na uwezo wa kusafirisha futi za ujazo 784 kwa siku bila mgandamizo na ukiwekwa mgandamizo utasafirisha futi za ujazo 1002 kwa siku.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment