Dar es Salaam.
Hatimaye, Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imetoa taarifa ya uchaguzi wa wanafunzi wa
kuingia kidato cha tano katika sekondari za Serikali na vyuo vya ufundi.
Katika uchaguzi huo,
wanafunzi 34,213 kati ya 34,599 waliofaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu
wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano, vyuo vya ufundi na Taasisi ya
Menejimenti ya Maendeleo ya Maji.
Uteuzi wa wanafunzi hao
ambao wanapaswa kuripoti shuleni Julai 29, mwaka huu unamaanisha kwamba
kutakuwa na upungufu wa wanafunzi wapatao 10,074 katika shule na vyuo hivyo vya
ufundi ambavyo vina uwezo wa kuchukua wanafunzi 43,757.
Upungufu huo unatarajiwa
kuwa mkubwa zaidi hasa ikizingatiwa kwamba baadhi ya wanafunzi hao watajiunga
na shule za sekondari za binafsi.
![]() |
| Naibu waziri na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo |
Aidha, kwa mujibu wa
matokeo hayo, ni wanafunzi 386 tu waliofaulu katika madaraja hayo ya kwanza
mpaka tatu ambao hawakuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano au vyuo vya
ufundi. Hao, wanaweza kujiunga na vyuo vya ualimu.
Kwa mujibu wa Kitabu cha
Takwimu cha Wizara ya Elimu (Best), mwaka 2012 wanafunzi 17,095 walichaguliwa
kujiunga na vyuo mbalimbali vya ualimu nchini.
Kutokana na takwimu hizo,
Serikali italazimika kuchukua wanafunzi wengi zaidi waliopata daraja la nne
kujiunga na vyuo vya ualimu kujaza pengo hilo.
Wanafunzi waliopata daraja
la nne kwenye mtihani wa kidato cha nne mwaka jana ni 124,260.
Mulugo alisema kuwa
wanafunzi waliopata daraja la nne pointi 27 watachaguliwa kujiunga na vyuo vya
ualimu endapo wataomba.
“Vigezo vya kujiunga na
kidato cha tano na vile vya vyuo vya ualimu ni tofauti, kidato cha tano mwisho
anatakiwa mtu mwenye pointi 25 na combination yake (uwiano wa masomo) iwe sawa,
ualimu ni pointi 27 wanafunzi wanaomba.
“Mwanzoni walikuwa
wanakwenda wenye pointi 28 lakini mwaka jana tukasema hapana iwe pointi 27 na
tutachukua kuanzia waliomaliza mwaka 2008 kama wataomba, kwa sasa hivi watu
wanaendelea kuwachagua,” alisema Mulugo.
Chanzo Mwananchi.


0 comments:
Post a Comment