Siku moja baada ya timu ya soka ya tanzania Taifa Stars kufungwa bao 1-0
dhidi ya Uganda katika mchezo wa kuwania
kufuzu fainali za michuano ya afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN)
mwakani,baadhi ya wanamichezo na mashabiki,wametoa maoni tofauti juu sababu za
timu hiyo kupoteza mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es
Salaam.
Wakati baadhi ya wanamichezo hao wakidai kwamba Stars imefungwa mchezo huo baada ya wachezaji
na wananchi kukataa tamaa na kupoteza mwelekeo kwa kuondolewa kwenye michuano ya kuwania kufuzu
kwenye kombe la dunia mwakani nchini Brazil,wengine wamedai timu hiyo
haikuibuka na ushindi kutokana na kukosa hamasa ya mashabiki na viongozi
uwanjani.
Aidha wanamichezo hao wamesema licha ya stars kutocheza chini ya
kiwango,matokeo ya mchezo huo si mwisho wa safari kwani muda bado upo kwa ajili ya kurekebisha dosari
zilizojitokeza na kuweza kubadili matokeo kwenye mchezo wa marudiano dhidi ya
The Cranes mjini Kampala Uganda ndani ya wiki mbili zijazo.




0 comments:
Post a Comment