Image
Image

MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NA SILLAHA HARAMU VINAHATARISHA USALAMA NA MAISHA YA VIJANA NCHINI KENYA.



Serikali ya Kenya imetuma vikosi maalum vitatu kupambana na hali ya kuongezeka kwa matumizi ya dawa za kulevya na uwepo wa silaha haramu, vinavyoathiri vijana wasiokuwa na ajira katika sehemu ya kaskazini mwa Kenya. 

Hatua ya serikali hiyo inatokana na wasiwasi waliouonesha wazee wa kikabila katika sehemu ya kaskazini mwa Kenya, waliosema matatizo hayo yanachangia kuvuruga usalama katika sehemu ya kaskazini mwa Kenya. 

Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwa na tatizo la kuongezeka kwa uhalifu katika eneo la Bungoma, ambako watu 30 waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa, katika eneo la Trans Nzoia watu 15 waliuawa, ikiwa ni pamoja na polisi watatu. 

Watu hao waliuawa na majambazi walionunua silaha haramu kutoka Uganda. 

Tatizo la umasikini na ukosefu wa ajira yanachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la uhalifu katika sehemu mbalimbali za Kenya.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment