Image
Image

,MWALIMU AMFUNGIA MWANAFUNZI WA SEKONDARI KWA ZAIDI YA SIKU 3 BWENINI BAADA YA KUMPA ADHABU KALI NA KULAZWA HOSPITALI YA RUFAA MKOANI IRINGA.




MWANAFUNZI wa shule ya sekondari ya Idodi iliyopo katika wilaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa Lusinde Nyaulingo amelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa baada ya kupewa adhabu ya viboko visivyo na idadi na mwalimu wake na kisha kufungiwa katika bweni kwa zaidi ya siku 3 ili kuficha uovu huo.

Tukio hili linakuja wakati ambapo kumekuwa na jitihada kubwa zikifanywa na serikali na asasi mbalimbali kukemea vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.

Ni mwanafunzi Lusinde anayesoma kidato cha tatu anaugulia maumivu makali baada ya kufanyiwana ukatili uliomsababishia majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake kufuatia kutuhumiwa kuiba simu ya mwanafunzi mwenzake hali inayomfanya kupoteza muda mwingi wa masomo wakati akiendelea na matibabu.

Lusinde anasema baada ya kuangushiwa kipigo hicho kikali, kilichodumu kwa zaidi ya masaa tatatu, alipoteza fahamu na kisha kufungiwa katika bweni kwa siku tatu, huku wanafunzi wenzie wakipigwa marufuku kufikisha taarifa ya ugonjwa kwa wazazi wa Lusinde. 

Kaka wa mwanafunzi Lusinde anauzungumziaje ukatili huu?
Kwa upande wake muuguzi katika wodi ya majeraha katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa  Bi Beatrice Tilya amethibitisha kumpokea mwanafunzi huyo.

Hata hivyo jeshi la polisi kupitia kamanda wake mkoa wa Iringa ACP Athmani Mungi amesema anafuatilia tukio hilo ili kuhakikisha haki inatendeka, kwa kumchukulia hatua za kisheria mtuhumiwa ikiwa pamoja na kumfikisha Mahakamani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment