Image
Image

MASUMU: WANACHAMA WA CCM KUWENI NA MAADILI MEMA NA KUACHA KULUMBANA NDANI YA CHAMA.




Chama cha mapinduzi CCM kimewaasa wanachama wake kuwa na maadili mema na kuacha tabia ya sasa ya kutuhumiana ndani ya chama wao kwa wao.

Hayo yamebainishwa na Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi wa Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam Rutami Masumu wakati wa Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika viwanja vya Yombo Vituka Jijini Dar es Salaam, ukiwa ni Mkutano wa kawaida kwa wananchi na kusoma taarifa ya utekelezaji ya ilani ya Uchaguzi wa mwaka 2010 uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete.

Amesema wanachama wanapaswa kukaa kwa ushirikiano na kufanya kazi za kichama kwa pamoja kwani kwa sasa kuna baadhi ya wanachama wanatumika kukivuruga chama, kitendo ambacho husababisha kutotekeleza malengo ya chama pamoja na ahadi walizotoa kwa wananchi wao.

Naye Mbunge wa Jimbo la Temeke Bw. Abas Mtemvu ameahidi kuendelea kuwasaidia akina mama na vijana waliojiunga katika mifuko  ya kujiimarisha kiuchumi ikiwemo VIKOBA, ambapo zaidi ya milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya kuwapa mikopo.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment