Image
Image

TAASISI YA CENTER FOR TRAING AND DEVELOPMENT INITIATIVE WALAANI VIASHIRIA VYA UVUNJIFU AMANI KATIKA MCHAKATO WA UPATIKANAJI WA KATIBA MPYA YA TANZANIA.



Umoja wa wanawake wa taasisi ya center for training and development initiative, CENTRADIN, wamelaani vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani katika mchakato unaoendelea hapa nchini wa kupata katiba mpya.

Akitoa tamko jijini DSM kuhusu mchakato wa amani katika kupata katiba mpya mkurugenzi mtendaji wa taassi hiyo kwa niaba ya wanawake wa umoja huo, SAUM RASHIDY amewaeleza waandishi wa habari kuwa uvunjifu wa amani ukitokea watakaoathirika ni wanawake, wazee, walemavu na watoto na kuongeza kuwa katiba haiwezi kupatikana kwa maandamano na vurugu ila kwa maridhiano ya kitaifa.
Aidha katika kuendeleza amani na maridhiano ya kitaifa wameomba viongozi wa vyama vya siasa na rais wakutane na kukubaliana juu ya mustakabali mzima wa kupata katiba nzuri na ya watanzania wote pamoja na kudumisha amani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment