Ripoti za Umoja wa Mataifa zimeeleza kuwa, zaidi ya
watoto 360 walio na umri wa chini ya miaka mitano wamefariki dunia nchini Niger
kutokana na utapiamlo.
Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa
Mataifa mjini Niamey amesema kwamba, vifo hivyo vya watoto wadogo vilitokea
kati ya mwezi Januari na Septemba mwaka huu katika eneo la Zinder.
Eneo hilo lenye watu wengi na masikini la Niger mara
kwa mara linakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana na ukame, tatizo
ambalo linawaathiri zaidi wanawake na watoto.
Kwa mujibu
wa Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF utapiamlo unasababishwa na
ukosefu wa virutubisho muhimu katika miili ya watoto, tatizo linalochelewesha
ukuaji na kudhoofisha mfumo wa kinga mwilini dhidi ya magonjwa ya kawaida ya
utotoni.


0 comments:
Post a Comment