Rais wa serikali ya
mpito ya Misri Adly Mansour ametangaza nia ya kuanzisha tena mradi wa nishati
ya nyuklia nchini humo.
Tangazo hilo la Mansour
limezua matumaini ya kufikiwa kwa ndoto ya mradi wa nyuklia nchini Misri.
Hata hivyo kuna baadhi
ya watu wanaopinga mradi huo kutokana na kuwepo kwa nishati endelevu kama vile
nishati ya jua na upepo.
Aidha Wengine pia wanatilia shaka uwezo wa
Misri kukamilisha mradi huo wakati inapokumbwa na msukosuko wa kisiasa na
matatizo ya kiuchumi.
Akizungumza na shirika la habari la China
Xinhua, mwenyekiti wa zamani wa kituo cha kitaifa cha usalama wa nyuklia nchini
Misri Bw Karim al-Adham amesema Misri inahitaji sana mradi huo kutokana na
upungufu wa umeme na kupungua kwa visima vya mafuta nchini humo.
Mwaka wa 2006, Misri ilitangaza kufufua mpango
wa nishati ya nyuklia kwa raia katika eneo la el-Dabaa kilomita 150 magharibi
mwa mji wa Alendandria, lakini wakazi wa huko walifika na kuharibu miundo mbinu
ya mradi huo.


0 comments:
Post a Comment