Image
Image

Watu 20 wafariki na wengine 23 hawajulikani walipo kufuatia ajali ya meli nchini Mali




Watu wasiopungua 20 wamefariki dunia na wengine 23 hawajulinaki walipo kufuatia ajali ya meli iliyotokea karibu na Mopti, mji wa katikati mwa Mali. 

Idara ya ulinzi wa usalama wa umma mjini humo imetoa taarifa ikisema, watu 210 wamenusurika, na idadi ya waathiriwa huenda ikaongezeka wakati shughuli za uokoaji zinapoendelea. 

Habari zinasema abiria wengi wa mashua hiyo walikuwa wakielekea vijijini mwao kwa ajili ya sikukuu ya kiislamu ya Tabaski Jumanne ijayo. 

Nahodha mmoja wa mashua amesema, ajali hiyo huenda ilisababishwa na ubebaji abiria wengi kupita kiasi.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment