Image
Image

MGOGORO WA KUKOPA MAREKANI, BENKI YA DUNIA YATAHADHARISHA.



                                         Jim Yong
Rais wa Benki ya Dunia, Jim Yong Kim ameonya kwamba Marekani imebakisha siku chache tu kabla ya kuingia kwenye hatari kubwa kwa sababu ya mgogoro wa Serikali ya nchi hiyo kukopa.

Amewataka watunga sera wa Marekani kufikia makubaliano ya kuongeza kiwango cha ukopaji cha Serikali ya nchi hiyo kabla ya siku ya Alhamisi ijayo.

Hazina ya Marekani itaanza kufilisika iwapo hakuna makubaliano kwa serikala ya Marekani kukopa kwenye masoko ya fedha.Bwana Kim ameonya kuwa hili linaweza kuwa janga la dunia pia.

Amesema kadri Marekani inavyozidi kushindwa kutoa maamuzi ya haraka, hali itakuwa mbaya zaidi kwa nchi zinazoendelea, ambapo amesema viwango vya riba vitaongezeka, imani itapungua na ukuaji wa uchumi utapungua kasi yake.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment