Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni PSPF, Adam Mayingu akitoa taarifa zamajukumu, mafanikio, changamoto na mipango ya mfuko kwa wadau wa mfukohuo
waliohudhuria kwenye hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa naPSPF.
DAR ES SALAAM.
Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma PSPF unatarajia kuwaingiza
katika mpango wa mafao watumishi wa tanzania wanaofanya kazi nje ya nchi, ili
kuwawezesha kupata mafao pindi wanapostaafu na kurejea nchini.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko huo Bw. Adam mahingu amefahamisha hayo wakati akizungumza wakati
wa chakula cha Usiku, kilichoandaliwa kwa ajili ya wadau wa mfuko huo jijini
Dar es Salaam.
Amesema
watumishi hao wataingizwa kwenye mpango wa mafao chini ya utaratibu mpya
ulioanzishwa wa uchangiaji wa hiyari, ambao umepanua wigo kwa kuruhusu wananchi
wote hata walio nje ya utumishi wa umma kujiunga na mfuko huo.
Kwa
mujibu wa Mkurugenzi Mkuu huyo, Mfuko wa PSPF ambao ulianzishwa Julai 1999,
umekuwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 20 kwa mwaka ambapo hadi kufikia sasa
umefanikiwa kuwa na amana zinazofikia thamani ya Shilingi Trilioni 1.25, zinazotokana na michango ya wanachama, uwekezaji na amana kwenye mabenki.

.jpg)
0 comments:
Post a Comment