Image
Image

WANANCHI WATAKIWA KUWA NA UZALENDO KATIKA KUTANGAZA UTALII WA TANZANIA KIMATAIFA.

 Geofrey Tengeneza Meneja Uhusiano wa Bodi ya Utalii (TTB) akitoa utambulisho wa mada zenyewe na malengo ya Warsha hiyo.

 Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii (TTB) Bw. Geofrey Meena akitoa maelezo mbele ya waandishi wa habari wakati akijibu maswali kwenye Warsha ya Mkakati wa kutangaza utalii wa Tanzania kimataifa iliyoandaliwa na Boodi hiyo na kuhudhuriwa na wahariri na waandishi mbalimbali wa vyombo vya habari pamoja na maafisa wa (TTB), Warsha hiyo imefanyika leo kwenye hoteli ya New Africa leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Philip Chitaunga Meneja wa Huduma za Utalii (TTB) na kushoto ni Sam Kasulwa Ofisa mawasiliano wa  (Tourism Confederation of Tanzania





 Na.Mwandishi Wetu Dar es Salaam.
Wananchi wameshauriwa kuwa na uzalendo katika suala zima la kuutangaza utalii wa Tanzania katika nchi za nje, ili kuwavutia watalii wengi kuitembelea Tanzania na hivyo kukuza pato la taifa na kuinuia uchumi wa nchi.

Ushauri huo umetolewa leo jijini Dar es salaam na Meneja wa Huduma za Watalii kutoka Bodi ya Utalii Tanzania TTB Bw. PHILLIP CHITAUNGA, alipokuwa akiwasilisha mada kwa wahariri na waandishi wa habari , juu ya mkakati wa utangazaji wa Utalii Tanzania na namna ya kuutangaza Utalii nje ya nchi.

Amesema Bodi ya Utalii kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Utalii Tanzania TCT wameazimia katika kutekeleza mkakati wa miaka mitano ijayo, watashirikiana kwa karibu na sekta binafsi , sekta za umma , pamoja na vyombo vya habari kuhakikisha wanatumia fursa zilizopo kuutangaza utalii , hivyo TTB na TCT wameiomba jamii kushiriki pia kikamilifu kuutangaza utalii wa Tanzania.

Amesema hivi sasa sekta ya Utalii inaingiza kiasi cha Dola za Kimarekani Bil. 1.7 kwenye uchumi wa nchi na kwamba katika kuhakikisha mkakati waliojiwekea unaimarika zaidi, TTB na TCT wameboresha mfumo wa utangazaji wa utalii kwa kutumia njia mbalimbali za mawasiliano zikiwemo vipeperushi,mitandao ya kijamii, na kwenye mikutano ya kimataifa.

Tayari Bodi ya Utalii Tanzania imeshaanza kukutana na makundi mbalimbali ya wananchi pamoja na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini ili kuhamasisha  wananchi kuwa wazalendo katika kuutangaza Utalii wa Tanzania ikizingatiwa kuwa hivi sasa utangazaji wa utalii ni wa watu wote kutokana na umuhimu wake.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment