Image
Image

Falcao aondoka uwanjani kwenda kutazama mechi nyumbani



Mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia anayechezea Manchester United, Radamel Falcao juzi aliamua kuondoka uwanjani kwenda kutazama mechi nyumbani baada ya kuwekwa benchi.

Nyota huyo aliye hapo kwa mkopo kutoka Monaco, aliachwa katika kikosi cha wachezaji 18 kilichoiwakilisha United dhidi ya Southampton na kuchapwa bao 1-0 nyumbani Old Trafford. Falcao anayelipwa Pauni 260,000 kwa wiki hakubaki uwanjani hapo na badala yake aliamua kuwasha gari lake na kuondoka uwanjani akitokomea kusikojulikana.

Kutojumuishwa kikosini kwa Falcao kuliwashangaza wengi baada ya Kocha wa Man United, Van Gaal kukiri kwamba mshambuliaji huyo hakuwa majeruhi.

Badala yake Van Gaal aliwaweka katika benchi walinzi watatu, Jonny Evans, Paddy McNair na Tyler Blackett huku katika safu ya ushambuliaji akimuweka benchi kinda James Wilson.

Falcao, ambaye ameanza mechi saba tu za Man United tangu alipojiunga kutoka Monaco, ameifungia Man United mabao mawili tu muhimu katika mechi zake tano zilizopita. Hata hivyo, Kocha Van Gaal amefafanua kwa nini alimuacha nje Falcao akidai kwamba zilikuwa sababu za kisoka zaidi na si vinginevyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment