Image
Image

Rais Kikwete na Mkewe mama Salma wawasili Mjini Maputo kuhudhuria sherehe ya uapishwaji rais mpya wa nchi hiyo Filipe Jacinto.


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
Coat of Arms              1 BARACK OBAMA ROAD,  
Coat of Arms11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili Maputo, mji mkuu wa Mozambique, usiku wa Jumatano, Januari 14, 2015, kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais mpya wa nchi hiyo, Mheshimiwa Filipe Jacinto Nyusi.   

Sherehe zinafanyika Independence Square, mjini Maputo leo, Alhamisi, Januari 15, 2015. Mheshimiwa Nyusi anakuwa Rais wa nne wa Mozambique tokea uhuru wa nchi hiyo mwaka 1975.
Kiongozi mwingine mkuu wa Tanzania aliyealikwa kuhudhuria sherehe hizo ni Rais wa Tatu wa Tanzania, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, ambaye amewasili akifuatana  na mkewe, Mama Anna Mkapa.
Ujumbe wa Tanzania kwenye sherehe hizo ni pamoja na Mama Salma Kikwete, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mahadhi J.Maalim,  Mheshimiwa Mohamed Abood Mohamed ambaye ni  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Philip Mangula ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM,  Mheshimiwa John Magale Shibuda ambaye ni Mbunge wa CHADEMA na Mheshimiwa Halima Dendegu ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu – Dar es Salaam.

15 Januari,2015

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment