Image
Image

Wanajeshi wa Kenya wawaua watuhumiwa watano wa Al-Shabaab

Wanajeshi wa Kenya jana waliwauwa watuhumiwa watano wa Kundi la Al-Shabaab katika mji wa pwani wa Lamu karibu na mpaka wa Kenya na Somalia.
Msemaji wa jeshi la nchi hiyo kanali David Obonyo amesema waasi walivamiwa na jeshi la Ulinzi la Kenya linalofanya kazi chini ya jeshi wa tume ya kulinda amani ya Umoja wa Afrika AMISOM, baada ya kutambua eneo lililotaka kuvamiwa umbali wa kilomita 6 hadi Basuba Kaunti ya Lamu.
 Msemaji huyo pia amefafanua kuwa baadhi ya wanamgambo wamekimbia wakiwa na majeraha, na operesheni ya kuwasaka ilianza mara moja.
Kanali Obonyo amesema katika tukio hilo wamepoteza mwanajeshi mmoja na wengine watatu waliojeruhiwa wanapatiwa matibabu.
Wanamgambo wamekuwa wakijificha katika maeneo ya msitu wa Boni ambako wanafanya mashambulizi dhidi ya wakazi na pia kuvamia mabasi kwenye mpaka na Somalia.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment